This website use cookies to ensure you get the best experience on our website
Kitabu hiki ni toleo lililoboreshwa la kitabu cha Mbinu Rahisi Za Kuandika Kitabu. Wakati nilipotoa kitabu cha Mbinu Rahisi Za Kuandika Kitabu nililenga kuwasaidia watu wanaotaka kuingia kwenye uandishi wa vitabu lakini hawana watu wa kushika mkono ili kufanikisha ndoto zao. Lengo bado ni lile lile isipokuwa nimeboresha zaidi na kufanya marekebisho fulani fulani baada ya kupokea maoni kutoka kwa wasomaji wengi waliosoma kitabu.
Katika toleo hilo jipya, nimeongeza vitu vingi ambavyo naamini, unapokisoma kitabu hiki utatoka ukiwa na nguvu mpya ya kuandika kitabu chako na hatimaye kutimiza ndoto yako ya kuwa mwandishi wa kitabu. Naandikaje kitabu? Ni swali ambalo nimejibu katika kurasa zinazofuata. Mimi naamini, kuandika kitabu ni ujuzi ambao kila mtu anawez kujifunza
Mwenye ndoto ya kuandika na kutoa kitabu ni wewe si mtu mwingine, mwenye ndoto ya kuuza nakala nyingi ni wewe na si mtu mwingine, na mwenye ndoto ya kuwa mwandishi aliyefanikiwa ni wewe na si mtu mwingine. Kwenye hatua yoyote uliyoko sasa; iwe kuandika, kutoa ama kuuza kitabu chako, kitabu hiki kitakuwa msaada kwako.
Unapoanza kusoma kitabu hiki unakuwa umeanza safari ya siku 25 za kuwa mwandishi aliyefanikiwa bila stress. Utafanikiwa kutimiza ndoto yako ya kuandika, kutoa na kuuza kitabu chako kwa mafanikio.
Upo tayari kuanza siku 25 za kuwa mwandishi aliyefanikiwa?
Upo tayari kuandika kitabu kitakachofika kwa msomaji wako?
Kwenye kitabu hiki nimeshughulika na mambo matatu;
Huishii tu kusoma kitabu. Upo huru kabisa kupata usaidizi kutoka kwangu, unapoendelea kusoma kitabu na ukaona kukwama kwenye jambo fulani, wewe nitumie meseji au nipigie, tutazungumza!
Upo tayari kuanza safari nzito ya kusoma sura sita zilizoshiba? Haya anza!